Taarifa iliyotolewa na mkurugenzi wa Kampuni ya
Mwandago Entertainment Ltd, Faustine Mwandago iliyosimamia ushindi wake
ngazi ya kanda ilisema kuwa mrembo huyo atawasili kwenye Uwanja wa Ndege
wa Kimataifa wa Kilimanjaro (Kia) saa 6:00 mchana.
Mwandago alisema kuwa mrembo huyo atapokelewa na
wenyeji wake, wakiwamo wazazi wake na kisha kupanda gari la wazi ili
kuwapa fursa wakazi wa Arusha kumshuhudia.
Alisema kuwa mara baada ya kuwasili Arusha atapelekwa moja kwa
moja nyumbani kwao, Sakina ili kushiriki hafla aliyoandaliwa na wazazi
wake pamoja na ndugu, jamaa na marafiki.
Wakazi wa Arusha wametakiwa kujitokeza kwa wingi
kumpokea mrembo huyo kwa lengo la kumpa moyo na kulikaribisha taji hilo
mara baada ya ukame wa muda mrefu wa kupata taji la Miss Tanzania.






0 comments:
Post a Comment