HADITHI,
HATUJAPENDA TUWE HIVI,
SEHEMU YA KUMI NA TANO (15),
MTUNZI Deo Young Massawe
MAWASILIANO, 0769297430.
sehemu ya kumi na tano (15)
Mwendo wa saa kumi na moja kamili Miriam aliamka akiwa na hamu kubwa ya kuwahi kazini ili ujumbe wa Genes uweze kufika mapema.
Baada ya kusali sala ya asubuhi, alichukua vile vipande viwili vya barua akavisoma kama desturi yake, alivisoma kila asubuhi na jioni na kila alipomaliza kusoma alijikuta akitokwa na machozi ila kwa siku hiyo machozi hayakumtoka kwani baada ya kusoma hiyo akichukua ile iliyokua inatumwa kwa Genes na kuibusu na kuiombea,
"baba naomba unisaidie huyu mwanaume nilieamua kumpenda kwa dhati aweze kunielewa, kwani sina nia mbaya nayeye naomba umfumbue macho aweze kuona upendo wangu kwake" Miriam aliomba akiwa kapiga magoti.
*******
"Saivi nishachelewa alafu nikienda na huku Aquiline nitachelewa zaidi" Josephat alijisemea kabla ya kutoka nyumbani,
"ila pale naweza pewa zawadi nzuri,sasa mwanamke akikwambia nakupa zawadi basi inawezekana ni penzi, ila sasa mwanamke mwenyewe ananituma kwa mwanaume wake sasa nitapewa nini?,ila ngoja nimpitie chapu nikimkosa sitamsubiri" Josephat baada ya kujishauri aliamua kupitia njia ambayo angemkuta Miriam.
********
"Waooh Genes leo umependeza sana" Angel alimtamkia Genes ambae walipanga wawahi shule ili wawe wanaongea pamoja kabla ya shughuli za usafi kuanza,
"hivi Angel mbona wewe umewazidi wanawake wote hapa shule ulimpa mungu zawadi gani,?au mungu alikuumba asubuhi na mapema maana hakukosea kitu" Genes alimpamba kwa maneno ya kumsifu hadi Angel akashindwa kusimama mwenyewe na hapo akamsogelea Genes na kumwegemea mabegani huku akilegeza macho,
"Angel angalia bhana tukionekana itakua magazeti shule nzima au ukute kuna mtu mwenye simu ya kisasa nakwambia badae tutakua Facebook" Genes alimnong'oneza Angel,
"sasa Genes nimeshindwa kuvumilia yani hapa nimepandwa na hisia za ajabu jaman nisaidie" Angel alimnong'oneza huku akipenyeza ulimi katikati ya sikio la kushoto la Genes,
"Angeeeeel acha jaman huoni huku ni shuleni" Genes alisema huku akijaribu kujitoa mikononi mwa Angel,
"sasa hata wanafunzi hakuna situfanye tu" Angel alimnong'oneza tena huku ulimi ukizidi kumtekenya masikioni.Genes alijisikia hali ambayo hajawahi kuisikia tangu azaliwe, alijihisi kama yupo katika sayari ya Mars ambayo anaisoma katika somo la Geography.
"Angel tuache alafu jumapili tukutane tufanye yetu basi" Genes alimbembeleza Angel kisha Angel akakubali kumwachilia.
Angel aliposikia kua jumapili atafanya mapenzi na Genes basi alimshukuru kwa kumsogolea kisha kumshika katika eneo la zipu ya suruali kama vile anataka kumfungua zipu,
"nini tena sasa Angel sinshakupa ahadi kua ni jumapili?" Genes alimsihi Angel atoe mkono wake sehemu hiyo,
"nataman niguse hii fimbo yangu ndo nisubirie kunichapa jumapili" Angel alimnong'oneza tena Genes huku akipitisha mkono ndani ya suruali ya Genes,
"weee acha" Genes aliruka nusura avunje kioo kwani alihisi msisimko wa ajabu ingawa alitamani aendelee kushikwa hapo pia aliogopa kwani tayari wanafunzi wengi washaanza kuingia shule.
Genes na Angel walitawanyika kila mtu kuendelea na shughuli zake huku wote wakiwa wanaisubiria jumapili kwa hamu hasa Genes ndio alikua kachanganyikiwa zaidi.
********
"Jaman huyu alinidanganya au vipi" Miriam alikua anaongea mwenyewe kama kichaa kwani alikua kasimama kwa mda mrefu bila kumuona Jesophat,
"au ndio yule" Miriam alisema baada ya kuona mwanafunzi aliekuja kwa mbali, na alivyoangalia kwa makini na kumtambua kua ni Jesophat,
"waooooh jaman nikasema umenidanganya kumbe unakuja jaman pole sana" Miriam alianza kuongea kwa sauti huku akiruka ruka kwa furaha hata kabla Jesophat hajamfikia,
"mmmh Genes na akili zake zote kumbe ndo maana kamkataa huyu kumbe ni kichaa kabisa, sijui namimi nimtoke maana anaweza niparamia hata aninyang'anye haka kamkoba kangu, ila kwa kua nishamfikia ngoja nimsikilize tu" Josephat aliwaza baada ya kuona Miriam anarukaruka bila kujielewa kabisa.
"Dada mbona kama una furaha sana" Josephat alianza maongezi kwa haraka,
"nimekusubiria sana hivyo kukuona lazima nifurahi" Miriam alijibu huku akitoa bahasha na kuibusu kisha kumkabidhi.
"hii hapa nisaidie kumpa alafu badae nitakusubiria hapa unipe majibu basi,nikusubirie saa ngapi ?" Miriam aliuliza,
"saa tisa kamili nisubiri ila vipi sasa kama akikataa kupokea," Josephat aliuliza,
"jaman asipopokea naomba nirudishie pia" Miriam alijibu ila ghafla alianza kutokwa na machoz kusikia mambo ya kurudishiwa,
"sawa basi nitafanya hivo" Jesophat alimjibu kwa huruma,
"chukua hii basi unywe chai,ila zawadi yako ni kubwa zaidi ya hii wewe nisaidie tu kwanza" Miriam aliongea huku akimkabidhi Josephat noti ya elfu tano.
Josephat hakuamini macho yake pale alipoona noti ya elfu tano,
"asante sana dada niatakufanyia kazi yako vizuri" Josephat alijibu kwa furaha na hali ya kutoamini,
"alafu usiiite tena dada, niite shemeji" Miriam alimtania Jesophat huku wakiagana.
"Sasa huyu mwanamke ana hela hivi alafu Genes anamkataa anamng'ang'ania yule mwanamke mweupe anaejipodoa anakua kama mdoli" Josephat aliwaza.
"uko wapi huo ujumbe uliosema unaagiziwa?" Genes alimuuliza Jesophat mara tu ya kuingia getini na kukutana,
"cheki sasa na wewe mikwara mingi eti jana unaongea kwa ubabe kua hutaki mazoea nae" Josephat aliongea kwa kicheko,
"we ungempitia uone namna ningeuchana chana na kuutupa" Genes nae alijibu kwa hasira,
"ninao bhna ngoja upo kwenye begi,nitakupa saa nne" Josephat alijisemea baada ya kuwaza kitu,kwani aliona uso wa Genes ni wakuonesha dhdhiri kua angechana au kuutupa ujumbe ambao angepokea.
Kengele ya saa nne ambayo iliashiria watu kupata pumziko kwa mda mfupi basi waliobanwa na haja mbalimbali ndio waliutumia kuenda sehemu husika pia waliokua na hela kidogo basi katika duka la shule walizidi kuongea jeuri, ambao walikua na baridi walilazimika kuota jua huku wakiwaangalia waliopanga foleni dukani sasa mda huo Angel aliutumia kumtembela Genes darasani kwake kwani tayari washaanza mahusiano.
"wee jihesabuni wote mpate kitu cha mia mia" Jesophat aliongea kwa sauti kubwa eneo la dukani kwani siku hiyo alikua na hela ambayo tokea aanze shule hajawahi miliki.
Baada ya kuitumia yote yeye na marafiki zake basi alielekea darasani na kuchukua bahasha ingine na kuweka huko karatasi isiyo na maandishi yoyote,
"hebu ngoja nimpime kwanza na hii nione" Jesophat alijisemea akielekea darasani kwa Genes huku bahasha kutoka kwa Miriam ikibaki ndani ya begi.
*******
"Angel vile vitu vya asubuhi ulijulia wapi maana hadi saivi nahisi furaha tu" Genes alikua katika mazungumzo na Angel kama kawaida yao kila ifikapo saa nne,
"naona kwenye movie za kizungu pamoja na kufundishwa kama hivi kwenye biology na hivo ni kidogo tu jumapili yani ndo hadi mtu azimie" Angel alimjibu,
"vipi mwanangu Genes naona uko na shem langu ila nakuomba kidogo tubonge" Josephat aliingilia na kuwakatiza maongezi,
"aah wivu tu sasa anamwitia nini" Angel alijisemea huku akivuta mdomo,
Genes na Josephat walisogea pembeni huku Genes akiingiza mikono mfukoni kuzuia kitu fulani ambacho aliona aibu wanawake kumuona katika hali ile.
"Nambie man" Genes alianza maongezi,
"hii apa barua yako" Josephat alimjibu huku akiingiza mkono mfukoni na kutoa bahasha, Genes aliipokea haraka na kuichana chana mbele yake,
"nilikuambia sitaki mazoea na huyo kenge aise chali angu mbona hatuelewani,au unataka urafiki wetu ufe nini man" Genes aliongea huku akimwangalia Angel ambae kwa wakati huo alilaza kichwa kwenye meza,
"haya basi poa tuachane na hayo mambo nilijua unatania kumbe ni hutaki kupokea ujumbe wake kweli" Josephat alimjibu huku akishangaa kwa kitendo cha Genes kuichana ile bahasha,
"nilihisi tu ndo maana nikamjaribu kwanza" Josephat alijisemea huku akitoka nje kwani kengele ya kuashiria mda wa kupumzika umeisha.
"sasa huyu shemeji angu itabidi nimrudishie tu hii bahasha yake nimweleze kilichotokea ili ajue hapendwi kabisa" Josephat alijisemea.
*********
"Dada Anitha leo saa nane kamili wote lazima tuwe wagonjwa na tuende hospitali" Miriam alimfuata Anitha na kumweleza hayo,
"sasa kama unaletewa majibu saa tisa kwa nini saa nane tuwe wagonjwa na tuende hospitali? hapo sijaelewa" Anitha alimuuliza Miriam,
"yaani namaanisha ikifika saa nane hapa kazini tudanganye tunaunwa ili tupewe ruhusa ya kuenda kupata dawa na hapo tusubirie majibu basi ili unisomee basi" Miriam alimuelewesha,
"sasa jaman tutaugua wote?wewe sema unaumwa ili Mimi nikusindikize hospitali maana watashangaa kuugua siku moja wote" Anitha alimpa wazo ambalo wote walikubaliana.
"Ndio yule nini?" Miriam alikua anafananisha kila mwanafunzi aliyemuona baada ya kudanganya anaumwa,
"Miriam hakika huyo mwanaume amekuchanganya sana akili" Anitha alikua anacheka tu maana Miriam alifanya kila aina ya kituko kila alipoona mwanafunzi yeyote alihisi ni Jesophat analeta majibu.
"Haya sasa ndo yuleeee" Miriam alisema baada ya kumuona Jesophat kwa mbali,
"tukatafute miwani au" Miriam aliongea utani huku akishusha sketi yake ili shem ake asije sema anavaa kimini.
Josephat nae alianza kuonesha uso wa furaha ili Miriam aondoe wasiwasi na wote walijikuta wakitabasamu kabla hata hawajaanza maongezi Miriam alianza kunyoosha mikono kwa mbali.
"Miriam acha basi nawe ukichaa wako siatafika hapa tu" Anitha alimsihi Miriam ambae alikua anaanza kutoka nduki kumfuata Josephat kwani aliona kama anachelewa kufika waliposimama.
Itaendelea,.
0 comments:
Post a Comment