Weusi wahairisha show

Author
Tokeo la picha la weusi
Weusi wamethibitisha  kuwa wameahirisha show yao ya Funga Mwaka iliyokuwa ifanyike jijini Mbeya Ijumaa hii kufuatia kifo cha rapper Geez Mabovu kilichotokea Jumatano jioni. Joh Makini amesema Geez alikuwa kama mtu wa familia yao. “Kusema na ukweli hatutaweza kufanya show ya Mbeya,” Joh Makini amesema kwa huzuni. “Ni kwasababu Geez ni mshikajiwetu, he is the part of the family, for the love of HIP HOP and respect hatuwezi fanya" Joh ameshirikishwa na Geez kwenye nyimbo zake tatu.

wakati huo huo Young Killer ametangaza kuaharisha kuachia video ya wimbo wake ’13’ aliomshirikisha Fid Q kufuatia msiba wa rapper Geez Mabovu uliotokea jana usiku. Video hiyo ilikuwa iachie Alhamis hii. Kupitia Instagram, Killer amesema video hiyo sasa itaachiwa Ijumaa ijayo. Kuna taarifa kuwa Geez anaweza kuzikwa leo kwao mjini Iringa.

0 comments:

Post a Comment