HADITHI,
HATUJAPENDA TUWE HIVI,
SEHEMU YA KUMI SABA (17),
MTUNZI Deo Young Massawe,
MAWASILIANO, 0769297430.
sehemu ya kumi na saba (17
"Yule sio Genes Kweli" Miriam alisema huku akisimama ili aweze kuona vizur mtu aliyemfananisha na Genes akivuka barabara kuelekea upande waliopo,
"naona ni yeye" Jesophat alijibu,
"na huyo msichana ni wawapi?"Miriam alisema huku akivua mkoba (kipima joto) aliokua ameubeba na kumkabidhi Jesophat,
"leo ni leo" alisema Miriam.
*********
"Vipi aise Chris"
"powa mkuu wangu Brown"
"huyu Angel ndo yupo na Genes leo"
"ndio jana sinimempa tahadhari?"
"nimemwambia asiopomuua leo tutaweka mambo yote hadharani"
"powa powa man wangu".
Yalikua mazungumzo ya kwenye simu kati ya vijana wawili akiwa ni Chris na Brown.Hawa vijana walikua ni watu wenye wivu na maendeleo ya mtu na walikua wanafunzi wenzake na Genes maendeleo ya Genes shuleni yaliwafanya wakose raha na kuamua kumtafutia mtu wa kumuua ndo hapo walimtumia Angel kufanikisha kazi yao.
Angel alikua ashawaua zaidi ya wanafunzi wawili ambao mmoja alimuua kwa kumpa sumu na mwingine alimnyonga alipokua akiwa nae chumbani kwa lengo la kufanya mapenzi,ingawa Angel alikua bado bikra.
Hivyo Chris na Brown walipojua kuhusu Angel kuua watu walimfuata siku moja na kumwambia,
"Angel hivi mbona unaua watu"
"jaman naombeni iwe siri yenu kua naua watu nawaomba msimwambie mtu,lolote mnalotaka nitawafanyia",
"ahaa sasa hatumtaki Genes huku duniani"
"sawa nitamuua ila iwe siri kubwa sana".
Baada ya hapo ndipo Angel alipoanzisha mahusiano na Genes ili iwe rahisi kumuua.
"Kweli huyu mwanaume nishampenda ghafla ila nitamuua tu ili nitimize lengo langu" ndiyo maneno Angel aliyosema asubuhi ya jumapili alipokua anaweka sindano ya sumu pamoja na wembe katika mkoba wake tayari kwa kuenda kukutana na Genes.
********
"Weweeeee! waacheee watoane nyongo,vita vya panzi ni furaha kwa kunguru,hahahaha lazima watoane chupi hapa".
Zilikua kelele za watu waliokua wakishuhudia pambano la Miriam na Angel,
"leo tutajua kati ya jogoo mweupe na mweusi nani kiboko ya mwingine" alisema dereva bodaboda mmoja.
Miriam na Angel walikua chini kila mmoja akijaribu kumvua mwenzake nguo,
"ananipiga maziwa!ananipiga maziwa" yalikua maneno ya Angel alipokua ameshikwa na kikunjwa,Miriam hakutaka mchezo alipiga mfano wa John Cena. Kwa wakati huo Jesophat alikua amemvuta Genes pembeni,
"mwanangu huu msala sasa" Jesophat alisema,
"aise huyu Miriam kumbe unatembea nae aise alafu unanipiga upepo tu pale shule,saivi umetoka nae wapi man wangu?" Genes aliongea huku akiwa na hasira za ndani,
"kweli huwezi amini tumekuja pale duka la vitabu nimemsindikiza hapo huyu Miriam"Jesophat alimjibu Genes,
" umekuja kununua kitabu?huyu kahaba anasoma wapi?"Genes alizidisha hasira,
"nitakuja kukuelezea vizuri" Jesophat alisema huku akiinama chini kuokota mkoba wa Angel uliokua umedondoka chini,
"oya utajuana nao" Genes alisema kisha kuondoka eneo lile huku akiacha pambano likiendelea,
"we utanambia leo umetoka wapi na bwana angu" Miriam aliuliza huku akimshushia Angel ngumi za macho,
"ni bwana angu we kahaba mweusi kama mkaa" Angel alijibu huku akijitahid kujifunika sehemu za siri ambazo zilikua nje kutokana na kuvaa sketi,yeye Miriam alihimili pambano kwa kuwa alivaa suruali.
"Hii sindano ni ya kazi gani pamoja na huu wembe?" Jesophat alijiuliza baada ya kutupa macho ndani ya mkoba wa Angel,
"hapana! hapa kuna kitu sio bure" Jesophat alizidi kujisemea, alitoa ile sindano na zile wembe akazificha katika mkoba wa Miriam aliokua ameushikilia.
"Nyie basi inatosha acheni vita" Jesophat alianza zoezi la kuwaachanisha ila hakuna alietemani kumwachia mwenzake.
"weee mkoba wangu" Angel alisema kwa sauti baada ya kuona Jesophat ndie kashikilia mkoba wake,alitumia nguvu zote kujitoa mikononi mwa Miriam na kuvaa Jesophat kisha kuchukua mkoba wake,
"jogoo mweupe ni mwoga" watu walipiga makelele,
"mimi siwezi pigania mabwana na sokwe" Angel alisema huku akifuta machozi,
*********
Genes baada ya kuondoka pale aliwaza mengi huku akimtupia lawana zote Miriam,
"yaani huyu Miriam sijui alinitokea wapi,kaniharibia kuenda kujua penzi la mke wangu Angel" aliwaza mengi na kuzidi kumchukia Miriam.
*********
"mama yangu hii sindano iko wapi?" Angel alijisemea Baada kuchungulia ndani ya mkoba wake,
'Itakua Jesophat kaichukua,na atakua amejitafutia matatizo mwenyewe" Angel alijisemea huku akimwangalia Jesophat machoni na hapo Jesophat akawaza kitu,
"Miriam tuondoke hapa" Josephat alimshika Miriam mkono na kutaka waondoke pale,
"ngoja kwanza tununue hicho kitabu cha mume wangu" Miriam alijibu huku bado akihema kwa hasira,
"apana tuachane na hayo, tutakuja siku nyingine saivi mambo yashaharibika" Josephat na Miriam waliondoka pale kuelekea kituoni ili waweze kurudi.
Katika kituo walichoenda kusubiri gari walimkuta pia Angel nae akisubiri gari ila alionekana kuwa na wasiwasi sana na kwakua alikua anasoma shule moja na Josephat basi alimwita na kumuomba nauli,
"mimi mwenyewe sina hata shilingi moja hapa" Josephat alimjibu kwa sauti ambayo Miriam alisikia.
"mpe mia tano kwenye ile chenchi" Miriam aliongea kwa sauti kuamuru Angel apewe nauli,
"asante sana" Angel alimjibu Miriam, gari ilikuja na wote wakapanda bila ugomvi wowote.
"Yaani huyu mwanamke amemponesha Genes sijui nitawaeleza nini akina Chris" Angel alikua akiwaza sana akiwa kwenye gari,
"ila huyu Josephat lazima afe maana kama kafanikiwa kuchukua hii sindano iliyokua ndani ya mkoba basi nitaweza gundulika" Angel aliumia sana kichwa na haraka alianza kupanga mbinu za kumuua Josephat ili asije kutoa siri ya yeye kutembea na sindano.
Itaendelea
0 comments:
Post a Comment