WAKALA WA SHETANI -08

Author

#Wakala_wa_Shetani -8-....

Alirudi haraka kwa mumewe aliyekuwa bado amelala huku amejikunja gubigubi kwa baridi la alfajiri.
"Mume wangu hawapo."
"Kina nani hao?" baba Sabina aliuliza.
"Si Mathayo na mkewe."
"Si nilikuambia."
"Kuhusu nini?"
SASA ENDELEA...

LIKE PAGE KIPANDE KIFUATACHO KISIKUPITE ONYESHA UPENDO MTU WANGU WA NGUVU #SHARE STORY NIPOST MWENDELEZO NASUBIRIA SHARE 250

"Huenda mtoto wao ni albino."
"Mmh, kweli hilo nalo neno," mama Sabina alimuunga mkono mumewe.
"Dawa ni kuitisha kikao na kuwaeleza watu."
"Itakuwa vizuri."
"Ila nimepata wazo kabla ya kukurupuka lazima tufanye uchunguzi wa kina."
Walikubaliana kwanza kufanya uchunguzi kabla ya kuitisha kikao. Baba Sabina aliamua shauri lile kulipeleka kwenye kikao cha kijiji.

Asubuhi ileile baba Monika aliwazungukia wajumbe wa almashauri ya kijiji na kuwaomba wakutane baadaye. Kikao kiliitishwa na kamati ya kijiji ilielezwa. Baada ya wajumbe kukusanyika, baba Sabina aliwaeleza alichowaitia.
"Ndugu wajumbe, nimewaiteni kuhusiana na kitu kimoja ambacho kimetokea si cha kawaida," alisema huku akitembeza macho kwa wajumbe wote waliokuwepo pale ambao walionekana wakimsikiliza kwa makini.
"Kipi hicho?"
"Si mnafahamu mke wa Mathayo alikuwa mjamzito?"
"Ndiyo, na mimba yake ilikuwa imebakiza muda mchache," alijibu mjumbe mmoja.

"Basi kuna taarifa zilizo rasmi kuwa mke wa Mathayo ameshajifugua, ila hajulikani mtoto wa jinsia gani. Sababu iliyonifanya niwaiteni ni tabia yao waliyoianza ya kutoka alfajiri na kurudi giza limeingia.
"Wasiwasi wangu kwa nini afanye vile hata kama hataki watu wajue mkewe amejifungua pia kuiona sura ya mtoto wao? Wasiwasi wangu huenda mtoto yule ni albino."
Albinoo!!" Walishtuka wajumbe wote.
"Ndiyo, kutokana na kauli aliyosikia mke wangu lazima tuwe na wasiwasi huo."
"Aah, albino, una uhakika na usemalo?" aliuliza mjumbe mmoja.
"Huo ni wasiwasi wangu, japo sina uhakika, nilikuwa nataka tuwatume vijana waende kule shamba ili wafuatilie wajue yule mtoto kama ni wa kawaida waachane naye, kama ni albino hapo ndiyo atatujua sisi tufanye nini."
"Inawezekana huenda hata mvua iliyonyesha ni laana ya kumkumbatia albino, kama ni kweli lazima apewe adhabu kali ambayo itakuwa fundisho kwa wanakijiji wote," alisema mwenyekiti.

"Kama ni kweli adhabu inayowafaa tuwafungie ndani ya nyumba yao kisha tuwatie moto na kufa kwa kuteketea kwa moto," mwingine alitoa wazo.
"Yaani kama ni kweli wafe kifo kibaya sana, hamuwezi kuamini mimi mifugo yote imekufa kwa mvua, kumbe kuna washenzi wanakumbatia laana," mjumbe mwingine alisema kwa uchungu.
"Nafikiri tusipoteze muda, majira ya saa tatu asubuhi vijana waelekee shambani kwa Mathayo ili kufanya uchunguzi. Walichaguliwa vijana sita na kupewa silaha tayari kwa kupambana na kitu chochote, wakaelekea shambani kwa Mathayo.

***
Mathayo, akiwa anaendelea kurekebisha shamba lake, aliponyanyua macho aliwaona vijana wakija kwa kasi wakielekea shambani kwake. Wasiwasi wake huenda kuna siri ya mtoto wao imevuja. Watu walikuwa mita mia saba kufika shambani.
Aliacha kila kitu na kukimbilia pangoni kumweleza mkewe kuwa mambo yameharibika, alipofika alimkuta mkewe akikoroma akionekana yupo kwenye usingizi mzito.
"Mke wangu...Mke wangu."

Kila alivyomwita kwa sauti ya chini hakusikia ilibidi amtikise kwa nguvu ili aamke.
"Mume wangu niache nilale nimechoka sana," Ngw'ana Bupilipili alisema bila kufumbua macho.
"Hapana mke wangu, amka, kuna watu wanakuja kumfuata mtoto wetu."
"Atiiii?" alishtuka na kuamka akiwa ametumbua macho.
"Kuna watu wanakuja upande wetu, inaonekana wanakuja kwetu tena si watu wa heri."
Kauli ile ilimfanya mke wa Mathayo ataharuki.

Alikusanya vitu muhimu na kutokomea kwenye msitu huku mumewe akibakia eneo lile kuangalia nini kinaendelea. Ng'wana Bupilipili alimfunga mwanaye madhubuti kifuani na kuanza kupanda milima kuondoka eneo lile kwa ajili ya kumnusuru mwanaye.
Wakati mkewe akiondoka eneo lile, Mathayo alitoka nje ya pango lile kuondoa ushahidi huku akimuomba Mungu mkewe azidi kukimbia na kumuokoa mtoto wao. Alijikuta akipata ujasiri wa ajabu na kuwa tayari kufa kuliko kumpoteza mtoto wake.
Itaendelea

0 comments:

Post a Comment