#Wakala_Wa_Shetani - 2
ILIPOISHIA:
Hawakuishia hapa walizunguka kila kona lakini hawakukuta kitu kingine zaidi ya vile vitu walivyoviona. Kutokana na kuonekana mtu yule ni vigumu kumkataka walatengeneza mtego na kuondoka.
SASA ENDELEA...
Siku ya pili walipofika walimkuta amenasa lakini akionekana kutaka kujinasua kwa kujitupa ovyo, walipomkaribia ili wamkamate aliwazidi nguvu kwa kutumia mkono mmoja aliweza kufanya uharibifu mkubwa kwa kuharibu vifaa ambavyo walivichukua kwa ajili ya kumrekodi mtu yule na kuua watu watatu.
Ilibidi wakimbie na kesho yake walikuja na bunduki yenye kutumia risasi ya kupunguza nguvu mwilini, apigwapo mtu huanguka lakini hafi. Ilibidi waende kwa taadhari kubwa wakiwa na baadhi ya wanajeshi wenye siraha kali kwa ajili ya kujihami.
Walifanikiwa kupiga risasi ya mgongo wakati akitaka kuwatoroka baada ya kuwashtukia. Alipopigwa alianguka chini na kupoteza fahamu, kufanikiwa kumchukua na kuondoka naye. Mtu yule baada ya kumuweka katika chumba ambacho wataalamu waliamini huenda atarudiwa na
akili ili waweza kumuuliza vitu kama atakuwa na kumbukumbu navyo na sababu ya kuishi kule porini kama mnyama.
Baada ya kumuua daktari ilibidi wawe makini naye huku wakijitahidi kufanya uchunguzi zaidi kujua sababu ya kuishi maisha yake. Mwanzo muda wote alikuwa amechukia lakini kila siku zilivyokuwa zikienda ndivyo alivyokuwa akibadilika. Katika chumba walichomuweka
walimwekea tivii ambayo walimwekea picha za katuni na za maisha ya watu wenye ulemavu wa ngozi waliokuwa wakiishi maisha ya upendo na watu tofauti.
Kuna siku wakati akiangalia katuni za Tom na Jerry aliangua kicheko mpaka machozi yakamtoka. Waliokuwa wakimfuatilia waliweza kugundua maendeleo makubwa kutokana na chombo kilichowekwa kurekodi matukio yake yote. Waliweza kumfungulia hata kukaa na watu bila kuonesha tabia za awali za kinyama na kuwachukia watu hata macho yake hakuangalia chini tena.
Taratibu aliweza kuwasiliana na watu kwa lugha ya Kiswahili cha kuungaunga chenye lafudhi ya Kisukuma. Baada ya kumrudisha kwenye afya yake, wana saikolojia walikaa naye kutaka kujua sababu ya yeye kuishi katika maisha yake. Baada ya kutulia kwa muda machozi yalianza kumtoka taratibu na kuweka michirizi juu ya mashavu yake kuonesha amekumbuka jambo lililouumiza moyo wake.
Baada ya muda mtaalamu aliyekuwa akimfuatilia toka mwanzo alimpa maji kwenye glasi na kumuomba ayanywe yote. Alikunywa maji yote na kutulia kwa muda kisha taratibu alianza kusimulia kisa kizima cha yeye kuishi porini kama mnyama kwa miaka yote hiyo bila kuonwa na mtu yeyote.
MIAKA 50 ILIYOPITA
Katika kijiji kimoja pembezoni mwa mji wa Mwanza karibu kabisa na ziwa Nyanza ambalo sasa hivi linaitwa Victoria. Majira ya saa mbili usiku Minza alikuwa akijigeuza katika kitanda cha kamba kilichotandikwa ngozi ya ng'ombe juu yale huku ameuma meno.
"Ngoshi wane…Mathayo."( Mume wangu…Mathayo)
Alimwita mumewe kwa sauti ya chini huku akifinya shuka kwa vidole vya mkono wa kushoto na mkono mwingine kujipigapiga kwenye paja kutokana na maumivu ya uchungu wa kujifungua.
Mathayo aliyekuwa ametoka nje kuvuta gozo lake aliisikia sauti ya mkewe kwa mbali. Aliliweka gozo lake pembeni ya mlango na kuingia ndani ambako kibatari nacho kilikuwa kisisinzia kutokana na kuishiwa na mafuta.
"Mwana Bupilipili ginehe hange?" (vipi tena?)
"Nalebona makanza gashika." (Muda umefika)
"Dogweta ginehe lolo?" (Tutafanya nini sasa?)
"Nene ango nalebyalela henaha do." (Mimi najifungulia hapahapa.)
"Yayah nke wana doganhwitane o mama Sabina." (Hapana mke wangu tukamwite mama Sabina.)
"Nale shaka hamo nagobyala mbelengw'elo bakomolaga" (Na wasiwasi wa kuzaa albino watamuua.)
"Ndoho odobyala mbelengw'elo hange." (Hapana hatuwezi kuzaa tena albino.)
"Nalemaga nilekage nabyale ngw'enekele olo odohayaga no bebe jaga"( Nasema sitaki niache nizae mwenyewe kama hutaki na wewe ondoka.) Ngw'ana Bupilipili alikuwa mkali baada ya kuona mumewe hamuelewi.
Mathayo hakuwa na jinsi alikubaliana na mkewe kumzalisha mwenyewe. Sababu kubwa ya mkewe kukataa kumwita jirani yao mama Sabina ili aje amzalishe ilitokana na desturi ya pale kijijini unapojifungua mtoto albino hutengwa kwa kufukuzwa kijiji alichopo au mtoto wako kuuawa kwa kupewa sumu.
Mwaka miaka miwili iliyopita ngw'ana Bupilipili alijifungua mtoto wa kike ambaye alikuwa albino uongozi wa kijiji uliwaeleza wachague kitu kimoja kufukuzwa kijijini au mtoto auawe. Ngw'ana Bupilipili alikubali kufukuzwa lakini mumewe alikubali mtoto auawe.
likuwa vita kubwa kati ya mume na mke baada ya mtoto wao kuuawa, ilibidi familia ya mke na mume kuingilia kati ikiwa pamoja na tambiko ili tatizo lile usitokee tena kwenye familia. Wao waliona ni mkosi mkubwa mtu kuzaaa mtoto albino.
Hali ile iliendelea kila siku kwa familia zote zilizozaa mtoto albino pale kijijini watoto wao kuuawa kwa kuonekana mikosi au kufukuzwa kijijini kama wakigoma mtoto wao kuuawa.
Wakiondoka na kwenda porini walitumwa vijana waliokwenda kumpora yule mtoto na kumuua. Wanawake wote kijijini walikuwa katika hali ya wasiwasi kwa kila mwanamke aliyebeba ujauzito alikuwa katika wakati mgumu mpaka atakapojifungua na kukuta mtoto wa kawaida.
Ngw'ana Bupilipili toka abebe ujauzito amekuwa hana raha kwa kumuomba Mungu usiku na mchana asizae tena mtoto albino hata kupanga siku ya kujifungua iwe siri kati yake na mumewe tu. Kila siku alimuomba Mungu asizae mtoto albino aliogopa kumpoteza tena japokuwa moyoni alijiapiza hata kuwa tayari mwanaye auawe na kuwa tayari kutengwa na kijiji na ayakaye muua lazima kwanza amuue yeye.
Ilibidi adanganye kwa kurudisha siku za ujauzito wake nyuma, kila alipoulizwa kuhusu ujauzito wake una miezi mingapi. Alirudisha miezi miwili nyuma ili atakapo jifungua ajue afanye kitu gani kama atajifungua mtoto albino.
Ndipo siku ya kujifungua ilipowadia hakutaka aitwe mtu yeyote kushuhudia anazaliwa mtoto gani kwa kuhofia siri yake kutoka nje kama atajifungua mtoto albino. Mumewe baada ya kukatazwa na mkewe asimwite mtu yeyoye aliamua kumsaidia mkewe kujifungua.
Itaendelea.
0 comments:
Post a Comment