MIMBA YA JINI -51

Author

Hadithi ya kusisimua #Mimba_ya_Jini -51-

#SOON NAACHIA #NEW_STORY #LIKE_PAGE USIPITWE NA STORY MPYA

ILIPOISHIA:
Asubuhi kabla ya kwenda kazini alimpa mkewe dawa aliyopewa usingizini na Shehna, baada ya mkewe kunywa alimuaga na kwenda kazini. Alipofika kazini kabla ya kuanza kazi mkewe alimpigia simu kumuambia hali yake ni mbaya kama mtu mwenye ujauzito wa muda mrefu.
SASA ENDELEA...

Alimwambia anywe glasi moja ya maji, mkewe alifanya hivyo, baada ya kunywa hali ilitulia lakini alikuwa amechoka sana, alipanda kitandani kulala. Alipoamka alijishangaa kukuta tumbo limekuwa kama ujauzito wa muda mrefu.Ile hali ilimshtua na kumpigia simu mumewe kumweleza kilichotokea.
“Usiogope hiyo ni hali ya kawaida huenda ujauzito huo uliingia muda mrefu, dawa niliyokupa imeufukua hivyo usiwe na wasiwasi. Kama vipi nenda hospitali ukapime hali yako.”
“Mume wangu hunipendi, tuliambiwa nini na Shehna?”
“Amesema sasa tunaweza kwenda.”
“Hapana tafuta ufumbuzi mwingine, sirudii kosa kidogo nife,” Husna aliogopa kurudia kosa.
“Usiwe na wasi mke wangu, Shehna ameruhusu, basi subiri nije nikupeleke mwenyewe.”
“Kama hivyo sawa.”
Mustafa aliacha kazi zake na kurudi nyumbani kumfuata mkewe na kumpeleka hospitali, alipofika nyumbani alishtuka kuona tumbo la mkewe limekuwa kubwa la ujauzito wa muda mrefu.
Lakini alificha mshtuko wake kwa kuhofia kumshtua mkewe na kuona kitu cha ajabu kimemtokea. Alimchukua na kumpeleka hospitali ambako katika kufanyiwa vipimo ilionesha ujauzito upo sawa.
Daktari alishangaa kukaa nao zaidi ya miezi mitano bila kufika hospitali, alimuonya asifanye vile tena kukaa na ujauzito kwa muda mrefu vile.
Baada ya maelekezo waliruhusiwa kurudi nyumbani akiwa amechoka kama ujauzito wote ulipitia hatua zote kufikia hatua ya kumchosha vile.
Walikubali na mumewe kukaa na siri ya chanzo cha ujauzito ule, ilikuwa tofauti na ujauzito anaoufahamu. Miezi miwili baadaye ujauzito ulipofikisha miezi saba kwa vipimo vya hospitali na maelezo ya Shehna, Husna alishikwa na uchungu mkali na kukimbizwa hospitali.
Kutokana na muda wa ujauzito ule, wengi waliamini ni maumivu ya tumbo tu, lakini kulionekana dalili zote za kujifungua.
Baada ya kufikishwa Husna aliendelea kuugungulia huku mkono mmoja umeshika kiuno na mwingine kichwa kutokana na maumivu makali ya uchungu.
Wauguzi walimkimbiza wodini wakiwa hawana uhakika kama siku ile ndiyo ilikuwa ya kujifungua. Baada ya kumfikisha walimpandisha kitandani huku Husna akiendelea kulalamika katika dalili zote za kujifungua. Ilibidi wampe huduma ya kujifungua, Husna alianza kusukuma mtoto, ghafla ulitoka moshi uliowafanya wote walewe na kusinzia.
Muda huo Shehna alimtuma jini wa kike kumpeleka mtoto wake wa kiume aliyekuwa akifanana na baba yake na kumweka pembeni ya Husna. Baada ya muda wote walishtushwa na kilio cha mtoto. Mtoto alikuwa amesha katwa kitovu kabisa na kusafishwa.
Hakuna aliyejua nani kafanya vile, kila mmoja aliamini mwenzake ndiye kafanya. Walimpa hongera mzazi kwa kupata mtoto wa kiume mwenye afya nzuri, hali ya mzazi nayo ilikuwa njema. Alipelekwa wodini kwa huduma zaidi. Baada ya taratibu zote, Husna aliruhusiwa kutoka hospitali na kurudi nyumbani na mwanaye ambaye kila aliyemuona alisema anafanana na baba yake.
Mustafa alijua kila kitu na kubaki na siri nzito moyoni huku amani akirudi nyumbani kwake kwa familia kufurahi na kusema mpaka wamtishe ndipo atafute mtoto. Japokuwa yule mtoto alikuwa wa kwake lakini hakuwa wa mkewe bali wa jini Shehna.
Siku nazo zilikatika muda nao ulisogea mtoto wa Shehna kurudi kwa mama yake.
Miezi mitatu ilipotimu, alitumwa jini kumfuata mtoto, akiwa katika umbile la kibinadamu mwanamke aliyevaa kiheshima. Jini Shaunani alitembea taratibu na kubisha hodi kwenye nyumba ya Mustafa.
Wakati huo mke wa Mustafa alimkuta amemaliza kumnyonyesha mtoto, alikwenda kufungua mlango na kumuona mwanamke mzuri aliyekuwa akinukia manukato kama anayotumia mumewe.
“Karibu.”
“Asante,” mgeni alijibu huku akiingia ndani.
Alipofika aliketi na kusema:
“Habari za hapa.”
“Sultani hajambo?” lilikuwa jina la mtoto ambalo Mustafa aliambiwa ampe mtoto na ndilo lilikuwa jina lake la ujijini.
“Hajambo.”
“Hebu nimuone.”
Husna bila wasi alimkabidhi mtoto jini Shaunani ambaye alikuwa mcheshi sana. Kutokana na ucheshi wake, alimzoea haraka Husna, hakuwa na wasiwasi alimuomba samahani.
“Samahani mgeni natoa vyombo vya mtoto.”
“Hakuna tatizo.”
Husna alirudisha vyombo vya mtoto jikoni na kurudi kumsikiliza mgeni, baada ya kukaa alimkaribisha tena.
“Karibu mgeni.”
“Asante,” kabla Husna hajaongeza neno simu iliita na kumshangaza kuitia chumbani wakati alikuwa nayo muda mfupi na hakurudi chumbani.
“Jamani hii ajabu simu nilikuwa nayo hata sijui niliondoka nayo muda gani kwenda nayo chumbani.”
“Labda umesahau haiwezi kujibeba yenyewe, kasikilize huenda ni shemeji,” jini Shaunani alisema.
Husna alinyanyuka na kwenda kupokea simu, kitendo cha kuingia chumbani tu. Jini Shaunani alitoweka na mtoto. Husna alipofika chumbani alishangaa kukuta simu haina ‘missed calls’. Alishangaa wakati alisikia simu ikiita kabisa hata mgeni alisikia.
Alitoka sebuleni alishangaa kukuta sebule tupu, hakuna mgeni wala mtoto wake.
“Mgeni...mgeni,” aliita kwa sauti.
Hakukuwa na jibu alitoka nje labda ametoka vilevile hakukuwa na jibu lolote, alijiuliza atakuwa amekwenda wapi.
Alitoka hadi nyumba ya pili labda wamemuona mtu akiwa na mtoto nao walisema hawajamuona. Alimpigia simu mumewe kumueleza kupotea ghafla kwa mwanaye.
Taarifa ile haikuwa ngeni kwa Mustafa, alijua mtoto keshachukuliwa na mama yake. Alirudi nyumbani haraka ili kumtuliza mkewe ambaye muda ule alikuwa amepagawa.
Alipofika alimkuta amepagawa akilia ovyo mikono kichwani. Husna alipomuona mumewe alimkimbilia na kumkumbatia na kuendeleza kilio.
“Mume wangu mwanangu ameibiwa!”

Itaendelea

BONGE LA STORY #SOON NAACHIA #NEW_STORY LIKE PAGE UWE WA KWANZA KUIPATA STORY YENYE MVUTO

0 comments:

Post a Comment