Hadithi ya kusisimua #Mimba_ya_Jini -50-
#SOON NAACHIA #NEW_STORY ILI UWE WAKWANZA KUIPATA STORY HYO #LIKE_PAGE HIII #SHARE #COMMENT #LIKE_PAGE UENDELEE KUWA KARIBU NAMI KIPANDE HATA KIMOJA KISIKUPITE.
ILIPOISHIA:
Mwezi mmoja kabla ya kujifungua Shehna alimweleza Mustafa kuwa muda ule anatakiwa kuwa sehemu maalum ambayo hatakiwi mtu yeyote kuingiza zaidi mzazi wake na mkunga tu. Pia alimweleza kuonana naye itakuwa baada ya miaka mitatu. Mustafa alikubaliana hakuwa na kipingamizi.
SASA ENDELEA...
Muda ulipofika Shehna alijifungua watoto mapacha watatu wa kike wawili na wa kiume mmoja. Ilikuwa ni furaha ilioje kufanikiwa kupata watoto toka kwa mwanadamu. Wakati wa kujifungua mawasiliano kati ya Mustafa na Shehna yalipotea, siku zote Mustafa alikuwa na hamu ya kuonana na Shehna lakini masharti yalimzuia.
Shehna baada ya matukio yote ya kuhatarisha maisha yake alikatazwa na wazazi wake asionekane mchana katika umbile la kibinadamu kwa muda wa miaka mitano nyongeza ya miaka miwili.
“Shehna kama mtoto umepata, sasa tulia kama ukiwa na shida na baba wa watoto wako tutamleta hukuhuku akiwa ndotoni baada ya miaka mitatu. Lakini kuonana naye akiwa na akili timamu ni baada ya miaka mitano.”
“Kwa hiyo nitarudi lini kama zamani?”
“Baada ya miaka kumi na tano ruksa kurudi tena katika umbile lako la kawaida na kutembea mchana kila mtu atakuwa amesahau yote yaliyopita hata watoto kumtembelea baba yao.”
“Sawa.”
Kuanzia siku ile Shehna aliendelea kulea wanaye kwa muda wote huo hakuweza kuwasiliana na Mustafa japokuwa alijua mzazi mwenzie alikuwa katika mawazo mazito ya kumtafuta mpenzi wake. Lakini aliheshimu maelekezo ya wazazi wake kwa kuhofia kwenda kinyume na kukutwa na matatizo.
Wakati Shehna akipewa maelezo na mama yake upande wa pili nyumba ya Mustafa ilikuwa inawaka moto baada ya wazazi wa Mustafa kumjia juu mtoto wao kutokana na siku kukatika bila kupatikana mtoto. Pamoja na kuwasihi wawe wavumilivu kwa vile mtoto ni siri ya Mungu hawakukubaliana naye.
Walitaka aachane na Husna kwa vile walikuwa wakitaka mjukuu, aliwaeleza mwaka ule ukiisha bila mkewe kushika ujauzito ruksa kuivunja ndoa yao. Wazazi wake walimkubalia na kumweleza mwaka ukikatika bila mtoto watampelekea mke nyumbani kwake.
Mustafa aliondoka kwao kichwa kikimuuma na kujiuliza zawadi aliyotaka kupewa na Shehna ya mkewe kushika ujauzito atapewa lini. Upande mwingine alimlaumu mkewe kwa kitendo chake kukiuka masharti ya Shehna muda ule wangekuwa na mtoto. Kibaya zaidi muda ule alikuwa amepoteza mawasiliano.
Alirudi nyumbani akiwa mnyonge sana, hakujua hatima ya ndoa yake kwa kuona mwaka unaweza kukatika kabla mkewe hajashika ujauzito na kufanya wazazi wake kumletea mke mwingine.
Usiku wa siku ile alichukuliwa na kupelekwa chini ya bahari, aliposhtuka alijiona yupo pembeni ya Shehna ambaye wakati huo hakuwa na tumbo kubwa. Ile ilimjulisha moja kwa moja tayari Shehna amejifungua.
“Pole mpenzi wangu.”
“Sijapoa kwa vile ndoa yangu inavunjika wakati wowote.”
“Najua ndiyo maana nimekuleta huku kabla muda wake, ilikuwa kazi nzito kuwashawishi wazazi wangu uje huku wakati ni juzi tu nimejifungua. Kwanza napenda kukupa hongera ya kuwa baba wa watoto wangu.
“Mungu kajalia nimejifungua mapacha watatu wawili wa kike mmoja wa kiume, wa kike ni wazuri kuliko mama yao na wa kiume ni mzuri kama baba yake. Kwa vile muda wangu wa kutoka huku bado. Niliwaomba wazazi wangu uje tujadiliane ili kuiokoa ndoa yako.”
“Nitashukuru.”
“Sasa kuna kitu nataka tukifanye iwe siri yetu, kwa sasa itakuwa vigumu kwa mkeo kushika ujauzito mpaka watoto wangu wafikishe mwaka. Kwa muda uliozungumza na wazazi wako lazima utapita na wazazi wako watavunja ndoa, najua na wewe unampenda sana mkeo.”
“Ni kweli.”
“Ni hivi nitampatia mkeo mimba tupu ambayo itakuwa ya muda mfupi kuliko mimba zote. Muda ukifika atakwenda kujifungua, kitakachotoka tumboni mwake kitakuwa upepo ambao utafanya wakunga wapitiwe na usingizi mfupi pamoja na mkeo. Sauti ya mtoto ndiyo itakayo washtua wakiamka watakuta mtoto pembeni ya mama yake.”
“Umesema atakuwa na mimba hewa na tumboni kutatoka hewa mtoto huyo atatoka wapi?”
“Mustafa nipo kwa ajili yakuokoa ndoa yako, kati ya wanangu nitamtoa mmoja ambaye wakati wamelala ataletwa na kuachwa hapo ili wakishtuka wajue amejifungua.
Nina imani baada ya hapo kesi itakuwa imeisha kwa wazazi wako kuamini mkeo siyo mgumba.”
“Kwa hiyo utamuachia huyo mtoto?”
“Hapana nitampa kwa miezi mitatu, kisha nitamchukua. Nahofia akianza kukua atakuwa na tabia za ajabu ambazo zitawachanganya hasa mkeo na majirani. Kwako atakuwa mwoga kwa vile ni baba yake lakini kwa mtu mwingine itakuwa vigumu kumsikiliza.”
“Utamchukua vipi?”
“Atapotea katika mazingira ya kutatanisha, usishtuke nitakuwa nimemchukua mwenyewe.”
“Sisi utatuachaje?”
“Najua mkeo ataumia kupotelewa na mwanaye, mbembeleze kwa vile baada ya muda mfupi atashika mimba ya kweli na kuzaa mtoto wa kwenu asiye na masharti.”
“Mmh! Sawa.”
“Mustafa usihuzunike kwa vile sina jinsi lazima nifanye hivyo ili kuokoa ndoa yako, nitakupa dawa utampa kwenye maji akinywa atakuwa na dalili zote za ujauzito. Najua atashtuka mwambie anywe maji glasi moja kuituliza.
Ujauzito huo utakuwa wa miezi mitano safari hii nendeni hospitali ili wazazi wako wajue ujauzito kumbe ni wa muda mrefu, baada ya miezi miwili atajifungua.”
“Sawa.”
Mustafa aliposhtuka akijikuta amelala kitandani kwake akiwa na dawa mkononi. Aliamka na kutulia kitandani kwa muda akikumbuka yote aliyoelezwa na Shehna, hakuwa na jinsi zaidi ya kukubali ili kuiokoa ndoa yake.
Asubuhi kabla ya kwenda kazini alimpa mkewe dawa aliyopewa usingizini na Shehna, baada ya mkewe kunywa alimuaga na kwenda kazini. Alipofika kazini kabla ya kuanza kazi mkewe alimpigia simu hali yake ni mbaya kama mtu mwenye ujauzito wa muda mrefu.
Itaendelea
#SOON NAACHIA #NEW_STORY #LIKE_PAGE UWE WA KWANZA KUIPATA STORY HYOOOO
0 comments:
Post a Comment