MIMBA YA JINI -37

Author

Hadithi ya kusisimuwa: #Mimba ya jini-37-

SHARE HADITHI UNIPE MOTISHA YAKUPOST VIPANDE VINGINE #LIKE PAGE HADITHI MPYA  ITAKAYO ANZA TENA UWE WA KWANZA KUIPATA

ILIPOISHIA:
Kwenye mkeka kulikuwa na wanawake watatu walikuwa wamejionyoosha na kuchukua nafasi kubwa. Baada ya kuketi na kuwasalimia kwa vile alikuwa mzoefu, alitoa simu yake kwenye mkoba na kumtumia ujumbe mganga kumjulisha yupo nje.
SASA ENDELEA...

Baada ya muda alitoka kijana mmoja mwenye umri isiozidi miaka 30 akiwa amevaa suruali ya jinsi na tisheti, ukimuangalia harakaharaka utajua brazameni.
Hakusema neno lolote, alimwita Sara kwa ishara ya mkono na kumwelekeza apite ndani.
Baada ya kuingia alikutana naye nje ya chumba cha uganga.
"Karibu."
"Asante, za siku?"
"Nzuri, umeadimika sana."
"Mambo mengi ustaadh wangu."
"Karibu ndani, maana nimefanya upendeleo."
"Najua ndiyo maana nikatuma ujumbe, niliogopa kupiga," Sara alisema huku akiingia ndani ya chumba cha mganga na kuketi kwenye mkeka.
"Mmh! Lete habari," mganga alisema.
"Habari nzuri, ile kazi ilikwenda vizuri yule bwana alirudi na alifanya kama ulivyosema, kwa sasa amekwenda nje kikazi, akirudi anakamilisha kila kitu."
"Sasa mbona hukurudi tumalize kazi?"
"Ndugu yangu kuna mambo yalinitokea ambayo sijawahi kutokewa toka nizaliwe."
"Mambo gani?"
Sara alianza kumueleza mauzauza yaliyokuwa yakimtokea kuanzia kupotea njia mpaka kuona nguruwe na sauti alizokuwa akisikia, pia wasiwasi wake kwa Shehna.
Mganga baada ya kumsikiliza alichukua kitabu cha uganga, karatasi na kalamu na kuandika vitu kwenye karatasi nyeupe kisha alifungua kitabu kuangalia alichoandika kilimaanisha nini kutokana na maelezo ya Sara.
Baada ya kusoma kwa muda alimuangalia Sara na kumuuliza swali;
"Unasema sauti ilisemaje?"
"Ilisema nisifuatilie mambo yasiyonihusu la sivyo nitageuzwa nguruwe kabisa."
"Kwa nini unafuatilia?"
"Kuna mambo yananitatiza."
"Ndiyo kuna kitu nimekiona hapa, inavyoonekana hakuna tatizo lolote zaidi ya kufuata maelekezo uliyopewa na ile sauti. Hutakiwi kupewa dawa yoyote zaidi ya kuisikiliza ile sauti. Kinyume cha vile mganga yoyote atakayejifanya anajua, moto utamuwakia."
"Kwa nini?"
"Hapana hakuna, tatizo unalo wewe kutaka kuingilia visivyo kuhusu achana nayo uwe salama, zaidi ya hapo utajuta kuzaliwa."
"Sasa utanisaidia vipi?"
"Msaada ni kuacha kufuatilia visivyokuhusu."
"Una maana ile hali haitatokea tena?"
"Ikutokee vipi nawe umeacha kufuata mambo yasiyokuhusu."
"Nitamjuaje anayenifanyia mchezo huo?"
"Sara kuwa muelewa, achana na mambo yasiyokuhusu, umjue ili iweje? Zaidi ya hapo sina msaada wowote wa kukusaidia."
"Hakuna kinga yoyote?"
"Kinga ya nini?"
"Inaweza kunitokea tena."
"Kama utayapuuza yale maneno na kujifanya unajua utageuzwa nguruwe na hakuna wa kukurudisha."
"Mmh! Sawa."
"Una lingine?"
"Kwa leo sina ila mwisho wa wiki nitakuja kwa ajili ya mambo yangu."
"Karibu sana."
Sara aliagana na mganga wake na kutokea mlango mwingine na kutoa nafasi kwa wateja wengine kupata huduma. Alitembea taratibu hadi kwenye kituo cha bodaboda na kukodi mpaka nyumbani kwake. Baada ya kufika kwake alikuwa mtu mwenye mawazo mengi kutokana na majibu ya mganga.
Alijiuliza kwa nini mganga alikataa kumsaidia, bado hakukata tamaa. Alipanga kwenda kwa mganga mwingine ili kupata ukweli aliamini kabisa mganga yule wa awali uwezo wake mdogo.
Kwa vile ilikuwa bado mapema, alichukua simu yake na kumpigia shoga yake anayeishi Kigogo.
Baada ya simu kuita kwa muda, ilipokelewa upande wa pili.
"Haloo Sara."
"Eeh! Mwaju za sahizi?"
"Nzuri, vipi shoga?"
"Eti mzee Gogo yupo?"
"Yupo, kwani vipi?'
"Nilikuwa nina shida naye."
"Kwa lini?"
"Leo hii."
"Mbona usiku?"
"Siwezi kulala mpaka nimuone kuna mambo yananitatiza."
"Mambo gani hayo ambayo lazima uende usiku huu."
Sara alimweleza sababu ya kutaka kuonana na mzee Gogo, baada ya kumsikiliza, alishusha pumzi na kusema:
"Mmh! Shoga una haki ya kwenda muda huu kwa mzee Gogo."
"Sasa tunafanyaje?"
"Nakusikiliza wewe."

Itaendelea
ENDELEA KUTEMBELEA PAGE HIII HADITHI HII IKIISHA NAWALETEA NYINGNE YENYE MVUTO ZAIDI CHAKUFANYA #LIKE PAGE HADITHI MPYA IKIANZA ISIKUPITEEE

0 comments:

Post a Comment