Hadithi ya kusisimuwa: #Mimba_ya_Jini-36-
ENDELEA KUONYESHA UPENDO KWA #KUSHARE HADITHI HII #LIKE_PAGE USIPITWE NA KIPANDE HATA KIMOJA
ILIPOISHIA:
Walikumbatiana kila mmoja akirudisha furaha yake, baada ya utulivu wa muda Shehna alimuomba Mustafa atoke nje mara moja. Alimruhusu hakuchelewa alirudi baada ya dakika mbili akiwa na vinywaji mkononi. Aliiweka juu ya meza na kwenda kwenye friji ndogo na kutoa glasi mbili.
SASA ENDELEA...
Alimimina kinywaji kile kwenye glasi na kumpa Mustafa.
"Karibu mpenzi."
"Asante," Mustafa alisema huku akikipokea.
Alikunywa funda mbili na kumumunya midomo kisha alisema:
"Aaah! Mpenzi kinywaji kitamu sana umepata wapi?"
"Nilituma mtu nyumbani alete wakati nakuja kukuaga."
"Ni kitamu hakika sijawahi kukinywa toka nitoke tumboni kwa mama yangu."
"Utazidi kuvipata maadamu tuko pamoja utakula vitamu zaidi ya hiki. Hii chupa utakuwa ukichukua glasi moja kila siku. Mpaka narudi nitakuta hujamaliza."
"Shehna wewe ni mtu muhimu sana katika maisha yangu, nitakupenda, nitakutunza na kukuheshimu siku zote za maisha yangu."
"Mustafa mpenzi mimi si mkaaji, nilikuja kukujulisha habari za ujauzito wangu na kukuaga."
"Sawa mpenzi nimekuelewa nami nitafuata yote uliyonielekeza bila kufanya makosa."
"Nitafurahi, kumbuka nakupenda sana Mustafa."
"Najua."
"Naomba usinisaliti."
"Nakuahidi sitafanya hivyo labda nife."
Walikumbatiana kwa muda kila mtu aliyasikia mapigo ya moyo wa mwenzake kisha waliachiana na kusindikizana nje. Alipofika mapokezi Shehna alimuaga Sara.
"Shoga nikukimbieni."
"Jamani, lini utakuja kwangu tuongee?"
"Tutapanga."
"Haya shoga sisi tunaendelea na kazi."
"Ila zingatia yote tuliyozungumza ili uishi kwa amani."
"Nitafanya hivyo."
"Haya kwa heri."
"Haya shoga."
Mustafa alitoka na Shehna hadi nje, alishangaa kutoona usafiri wowote nje uliomleta, alijiuliza ataondokaje.
"Shehna unatumia usafiri gani?"
"Utanisindikiza mpaka njia panda kuna gari la nyumbani litanipitia."
"Sawa." Waliingia kwenye gari la Mustafa na kumpeleka mpaka sehemu aliyotaka na kumwambia.
"Niache hapa kuna gari litanipitia sasa hivi."
"Sawa."
Mustafa alisimamisha pembeni ya barabara kwenye mti wenye kivuli na kumwambia:
"Haya mpenzi nenda salama daima nitakukumbuka."
"Jamani Mustafa si mwezi tu."
"Kwa umpendaye siku moja mwaka."
"Najua, hata mimi nilipenda ujauzito huu niulee na wewe, lakini mila lazima nifanye tambiko bila hivyo naweza kupoteza wanangu."
"Haya mama naheshimu kwa vile ni kwa ajili yetu."
Waliagana kwa kukumbatia kwa muda kisha Shehna aliteremka kwenye gari na kwenda kusimama chini ya mti, Mustafa aliondoa gari kurudi ofisini. Siku ile Shehna hakutaka kuondoka kwa mtindo wake wa kutoweka ghafla, alihofia baada ya utata uliojitokeza kwa Mustafa ilibidi afanye vile ili wajue ni kiumbe cha kawaida wala si kama wanavyomdhania. Baada ya kumuona Mustafa ametoweka naye alitoweka ghafla na kurudi chini ya bahari.
***
Sara baada ya kumaliza kazi aliondoka kuelekea kwa mganga wake ili apate ukweli wa kitu kilichomsumbua. Ili kukwepa foleni alichukua bodaboda kuelekea kwa mganga Vingunguti kwa vile walitumia usafiri ule waliweza kukwepa foleni za barabarani na kutumia nusu saa kufika kwa mganga.
Kwa vile hakutaka dereva wa bodaboda ajue anakwenda wapi, aliteremka mbali kidogo na nyumba ya mganga ambayo ilikuwa vigumu mtu kujua mpaka aelekezwe. Alitembea hatua kama hamsini na kutokea uani kwa mganga, alikuta wateja zaidi ya nane waliokuwa chini ya mti, wanawake sita pamoja na yeye jumla wakawa saba na mwanaume mmoja alikaa kwenye benchi palipokuwa na nafasi.
Kwenye mkeka kulikuwa na wanawake watatu walikuwa wamejionyoosha na kuchukua nafasi kubwa. Baada ya kuketi na kuwasalimia kwa vile alikuwa mzoefu alitoa simu yake kwenye mkoba na kumtumia ujumbe mganga kumjulisha alikuwa nje.
Itaendelea
NAKUELEWA SANA MTU WANGU WA NGUVU #SHARE HADITHI HII TWENDE SAWA #LIKE PAGE ONYESHA UPENDO.
0 comments:
Post a Comment