MRISHO NGASSA AWA MMFUNGAJI BORA AFRIKA LAKINI MKONO MTUPU

Author
Mshambuli
aji wa Dar Young Africans,Mrisho khalfan Ngassa amepata zali Afrika,Baada ya kumaliza kinara wa mabao katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika,Licha ya klabu yake kuaga mashindano Alfajiri kabisa,Ngasa amemaliza kinara baada ya kufunga mabao 6 na kufungana na Ndombe Mubele wa AS Vita Club ya Jamhuri ya Demokrasia ya Congo,Haythem Jouini wa Esperance de Tunisi ya Tunisia na El Hedi Belameiri wa Es Setif ya Algeria.Ni baada ligi ya Mabingwa Afrika kufika tamati wikiendi iliyopita na Es Setif kutangazwa mabingwa wapya wakibebwa na bao lao ugenini kutokana na matokeo ya sare ya 1-1 mchezo wa Algeria na sare ya 2-2 mchezo uliochezwa kinshasa.Ngassa aliyafunga mabao hayo katika raundi ya kwanza walipocheza na Komorozine ya Comoro mchezo wa kwanza walishinda 7-0 na marudiano walitoka kifua mbele kwa ushindi wa mabao 5-2.Yanga ilitolewa na Al Hahly ya Misri kwa penalt 4-3,Lakini Ngassa hawezi kupewa zawadi kwa vile wamefungana kiutaratibu hata mchezaji akishinda tuzo hiyo CAF huitoa  kwa  klabu yake                                                                                                                        .Tokeo la picha la mrisho ngassa photo
 

0 comments:

Post a Comment