Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco),
Felchesmi Mramba amesema kesho na keshokutwa hakutakuwa na huduma ya
ununuzi wa umeme kupitia Luku nchi nzima.
Hatua hiyo inatokana na kubadilisha mfumo wa uuzaji na usambazaji wa umeme kwa wateja kutoka Luku kwenda mfumo mpya wa 3E.
Alisema
hayo juzi wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini hapa kuhusu
taarifa zilizosambaa kuwa huduma hiyo haitakuwapo kwa siku saba na
kufafanua kuwa huduma hiyo itakosekana kwa saa 24 tu.
“Mfumo
huu wa Luku haukidhi vizuri mahitaji ya wateja kutokana na kushindwa
kuhudumia wateja wengi kwa wakati mmoja, lakini mfumo 3E unaweza
kuhudumia wateja wengi zaidi,” alisema Mramba.
Amewaomba
wateja kuwa wavumilivu katika kipindi hicho cha kufanya marekebisho
hayo ya mfumo. Mramba alisema mfumo wa 3E utaongeza ufanisi, ikiwa ni
pamoja na wateja wote kupata huduma kwa urahisi na haraka kuliko hapo
awali.






0 comments:
Post a Comment