Iko hivi; Yanga ilimtanguliza mjumbe wake wa kamati
ya mashindano, Samuel Lukumay Jumanne iliyopita ambapo alipotua tu
kwenye Uwanja wa Ndege wa Bulawayo akagundua kitu.
KATIKA kuthibitisha kwamba imepania kufika
kwenye levo nyingine tofauti msimu huu kwenye michuano ya kimataifa,
Yanga imeshusha mashushushu wake Zimbabwe ambao wamebaini mitego ya
hatari waliyokuwa wamewekewa na wapinzani wao ambao ni FC Platinum.
Iko hivi; Yanga ilimtanguliza mjumbe wake wa
kamati ya mashindano, Samuel Lukumay Jumanne iliyopita ambapo alipotua
tu kwenye Uwanja wa Ndege wa Bulawayo akagundua kitu.
Wale jamaa wameweka mtego kwamba Mtanzania yeyote
atakayetua uwanjani hapo wapate taarifa, unajua alichowazuga ni kuwa
yeye ni mfanyabiashara Mtanzania anaishi Afrika Kusini hakai Zimbabwe
anapita tu.
Akawachota akili wakajisahau akaingia mjini
akaanza kufanya yake akakutana na Watanzania wanaoishi Bulawayo wakampa
maelezo muhimu na jinsi watakavyoisaidia Yanga kuanzia kwenye misosi na
kila kitu. Lakini kila akizunguka mitaani pamoja na Wabongo wengine
hawazungumzi Kiswahili ili wasishtukiwe. Kwahiyo kinachofanyika ni
kwamba Yanga ikitua leo itafikia Bulawayo halafu kesho asubuhi itakwenda
Zvishavane kwa basi asubuhi ambapo itafikia kwa kushtukiza kwenye
hoteli yoyote ili kupumzika kidogo na kupata msosi halafu wakiamka
wanapilitiza hadi uwanjani.
Yanga wameafikiana kwamba mbinu hiyo ndiyo pekee
inayoweza kuwanusuru na wamepanga kupiga chini hoteli zote
walizoandaliwa na wenyewe wao karibu na eneo la uwanja.
Yanga wamegoma kufikia moja kwa moja katika mji
huo ambapo sasa kikosi hicho kitaweka kambi ya saa kadhaa jijini
Bulawayo kabla ya kwenda Zvishavane ambako kuna umbali utofauti wa
kilometa 170 na watakaa kwenye basi saa mbili kabla ya kufika katika
uwanja wa Mandava unaochukua jumla ya mashabiki 10,000.
Katibu Mkuu wa Yanga Jonas Tibohora alikiri
kupatiwa taarifa hizo ambapo pia alisema wamepata taarifa kuhusu
Platinum kuwa wapo katika mazoezi makali wakitaka kulipiza kisasi na
tayari makocha wana taarifa zote.
“Unajua wale kule ligi yao ndiyo imeanza sasa
hawataki kuweka nguvu nyingi katika ligi ambayo itachukua muda mrefu,
wameona nguvu kubwa waiweke katika mchezo wetu kwa kuwa ushindi wa mabao
5-1 tulioupata hapa umewaweka katika wakati mgumu viongozi wao na hata
makocha,”alisema Tiboroha.
“Kuna kiongozi wao alinipigia simu wakitaka kujua
tunakwenda lini ili watuwekee hoteli nikawaambia watulie kwa kuwa bado
tunajipanga, tunataka kuwa makini katika mchezo huu kuepusha kutolewa
kwa makosa ambayo tungeweza kuyakwepa, tumejiandaa vyema kiuchumi
kukabiliana na wenzetu hawa.” alisema.






0 comments:
Post a Comment