Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete
alfajiri ya jana, Jumamosi, Novemba 8, 2014, alifanyiwa upasuaji wa tezi
dume (prostrate) katika Hospitali ya Johns Hopkins iliyoko Baltimore,
Jimbo la Maryland, Marekani.
Rais Kikwete amefanyiwa upasuaji huo baada ya madaktari waliomfanyia
uchunguzi wa afya yake kujiridhisha kuwa Rais alikuwa anahitaji matibabu
ya aina hiyo. Upasuaji huo uliofanyika alfajiri na kuchukua kiasi cha
saa moja unusu, umefanyika salama na kwa mafanikio makubwa. Hali ya
Mheshimiwa Rais Kikwete inaendelea vizuri, bado yuko wodini akiendelea
kuwa chini ya uangalizi wa madaktari na kupatiwa tiba.
Wananchi wataendelea kupewa taarifa sahihi kuhusu hali ya Rais Kikwete kwa kadri zitakavyokuwa zinapatikana.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment