Hadithi ya kusisimua #Mimba_ya_Jini-24-
ENDELEA #KUSHARE HADITHI HII NIPOST MWENDEKEZO WAKE ONYESHA UPENDO KWA KULIKE PAGE HII KIPANDE KINACHOENDELEA KISIKUPITEE #LIKE_PAGE
ILIPOISHIAJANA :
Vijakazi na watwana waliingia katika kazi ya usafi iliyochukua dakika tano kila kitu kilikuwa safi ndani. Kilibadilishwa kila kitu na kuwekwa pazia nzuri la halili na kuifanya ofisi ipendeze mara dufu. Baada ya kufanya usafi walipiga magoti mbele ya Shehna na kusema.
SASA ENDELEA…
"Mtukufu mwana wa Mfalme wa jini la bahari ya dhahabu tumemaliza kazi, kama kuna kasoro tupo tayari kwa adhabu yoyote kutoka kwako."
"Hapana nawamini."
"Asante mwana wa mfalme."
Shehna hakuwa na shida ya kukagua kwa kuamini majini walikuwa wakijua usafi kuliko mwanadamu.
"Nimefurahi kwa yenu nzuri, mnaweza kuondoka."
Kufumba na kufumbua vijakazi na watwana walitoweka na kumuacha Shehna alifurahia hali nzuri ya kupendeza ya ofisi. Alitoka nje na kumwita Mustafa aliyekuwa akizungumza na mlinzi. Alikwenda ndani na kuishangaa ofisi ilivyopendeza tofauti na siku zote.
"Duh! Kazi hii imeifanya peke yako?"
"Umemuona nani akinisaidia?"
"Hongera sana."
"Asante, ila kama Sara hatatokea na kesho funguo iache mlangoni, nitakuwa nawahi mapema kufanya usafi kabla hujafika mpaka atakaporudi kazini ."
"Nitafanya hivyo."
"Mustafa mimi si mkaaji ilikuja kukushukuru wa mapenzi yako matamu, hakika leo nimefaidi usichana wangu kwa kupata penzi lililokamilika. Nakuahidi baada ya kushika ujauzito nitakupatia zawadi kubwa sana."
"Wala usihofu, lakini nina wasiwasi wa kuharibu masharti yako."
"Wala usiwe na wasiwasi, asubuhi umenilaisishia kufanya mambo yetu bila mkeo kukusumbua. La muhimu kufanya yote kama niliyokuelekeza."
"Nitafanya hivyo."
"Basi nikuache uendelee na kazi."
"Nashukuru."
Walikumbatiana kisha Shehna aliondoka na kumuacha Mustafa alimsindiza kwa macho.
***
Wiki nzima ilikatika bila kuonekana kwa Sara huku Shehna akiendelea kufanya usafi kila siku na kuifanya ofisi izidi kupendeza. Kwa hali ile ilifikia hatua ya Mustafa kuomba Sara isirudi tena kutokana na usafi uliokuwa ukifanywa na Shehna uliifanya ofisi yake isifikiwe kwa kila aliyeingia na kutaka kupatiwa mtu mwenye uwezo wa kufanya usafi kama wa ofisini kwake.
Wakati wote huo kila siku Shehna alikwenda nyumbani kwa Mustafa na kufanya naye mapenzi kitandani kwake huku mkewe akiwa amepitiwa usingizi. Siku zote alifuata masharti aliyopewa kuyafanya kabla ya kulala. Zoezi kubwa kwake lilikuwa kumpaka mafuta mkewe ambayo humfanya alale mpaka asubuhi bila kugeuka na kuacha wafanye mambo yao bila yeye kujua kinachoendelea.
Mustafa alifanya vitu vyake siku zote kwa umakini mkubwa kwa vile mkewe hakuweza kukutana naye tena kimwili baada ya kuelezwa na Shehna ili aweze kupata mtoto huku akiendelea kutumia dawa alizopewa. Hata kulala sehemu ya ukutani hakulazimishwa kwa vile lilikuwa moja ya masharti ya dawa.
Siku zote alifanya kama alivyoelekezwa, lakini siku moja alirudi nyumbani akiwa amechoka sana na kusahau kumpaka mafuta mkewe kwa kuamini aliisha mpaka. Usiku kama kawaida Shehna aliingia ndani na kunyanyua Mustafa na kwenda naye bafuni kuoga baada ya kuoga alirudi kitandani na kuanza kuandaana kisha waliingia kwenye tendo.
Hatua ya awali iliisha kila mmoja alifurahia penzi la mwenzake kisha walipumzika kwa muda ili kujiandaa kwa hatua nyingine. Shehna kama kawaida alimpa Mustafa maji ya kunywa yaliyomrudishia nguvu na kurudi tena bafuni kuoga na kuingia hatua ya pili. Mapenzi yalipopamba moto Shehna aligugumia kimapenzi kwa kuusifia uwezo wa Mustafa kimapenzi.
Kwa vile mke wa Mustafa hakupakwa mafuta ya kumlaza, sauti ya kulalamika kimapenzi ilimshtuka usingizini.
Itaendelea
KAMA BADO UJA#LIKE_PAGE LIKE SASA ILI MWENDELEZO WA HADITHIII HIII USIKUPITEEE #SHARE NIPOST KIPANDE KINACHO FUATAAA,
0 comments:
Post a Comment