Elimu ya msingi kutolewa bure Zanzibar

Author

Rais Ali Muhammed Shein wa ZanzibarSerikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) imefuta ada ya wanafunzi wa shule za msingi, ikiwa ni utekelezaji wa dhamira ya mapinduzi ya kuwapatia wanafunzi wote elimu bure, kama ilivyoasisiwa na Rais wa Kwanza wa Zanzibar, Abeid Amaan Karume. Uamuzi huo ulitangazwa rasmi jana na Rais Ali Mohamed Shein, wakati akihutubia wananchi katika uwanja wa Amaan katika kilele cha maadhimisho ya miaka 51 ya Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964. Rais Shein alisisitiza kwamba, kuanzia sasa Serikali inafuta ada ya wanafunzi wa shule za msingi walizokuwa wakitoa wazazi, ikiwa ni malengo ya kutekeleza dhamira ya Mapinduzi ya Zanzibar ya kuwapatia wanafunzi wote elimu bure, kama ilivyoasisiwa na hayati Karume na kutangazwa Septemba 23, mwaka 1964. Aidha Dakta Shein amebainisha kwamba, mafanikio makubwa yaliyopatikana katika sekta za elimu, afya na usambazaji wa nishati ya umeme, ni mambo ambayo yalikuwa moja ya vipaumbele, vilivyowekwa katika Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964.

0 comments:

Post a Comment