FIGO VIONGOZI WA AFRICA WANAFIKI

Author
Mgombe nafasi ya uraisi wa shirikisho la soka duniani FIFA Luís Filipe Madeira Caeiro Figo amepasua ukweli wa unafiki uliokithiri barani Afrika kuelekea katika uchaguzi wa uraisi utakaofanyika mjini Zurich nchini Uswiz mwezi ujao.
Figo ambaye anaonekana kuwa mpinzani wa karibu wa Joseph Sepp Blatter katika kinyang’anyiro cha uraisi wa FIFA, amepasua ukweli huo alipozungumza na vyombo vya habari wakati wa mkutano mkuu wa CAF ambao jana uliamua nchi ya Gabon kuwa mwenyeji wa fainali za Afrika za mwaka 2017.
Figo amesema baadhi ya viongozi wa soka barani Afrika wamekua wakisambamba propaganda kwa viongozi wenzao na kuwahimiza wampigie kura Blatter, jambo ambalo limemkera sana yeye kama mgombea.

0 comments:

Post a Comment