ACT WAANZA ZIARA MIKOANI

Author
Wakati joto la uchaguzi likiendelea kupanda, Chama Cha Alliance for Change and Transparence (ACT-Tanzania), kimeanza ziara ya kujijenga katika mikoa ya 10 nchini.
 
Taarifa ya ACT iliyotumwa kwa vyombo vya habari jana ilieleza kuwa ziara hiyo ya siku 10 inaanza leo mkoani Ruvuma na itamalizika Aprili 19, mkoani Mara.
 
Taarifa hiyo ilieleza kuwa baada ya Ruvuma ACT itaelekea Njombe, Iringa, Morogoro, Dodoma, Singida, Tabora, Shinyanga, Mwanza na kisha Mara.
 
Chama hicho kimeanza harakati za kujitangaza siku chache baada ya kuzinduliwa rasmi na baada ya aliyekuwa mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe, kujiuzulu ubunge na kujiunga nacho.
 
Zitto ambaye ndiye msemaji mkuu wa ACT-Tanzania alijiunga rasmi na chama hicho Machi 21, mwaka huu na kukabidhiwa kadi namba 007194 huku akitazamiwa katika ziara hiyo kuwa miongoni mwa viongozi waandamizi watakaoshiriki mikutano ya hadhara itakayofanyika.

0 comments:

Post a Comment