Hadithi ya kusisimua #Mimba_ya_Jini-14-
Mtunzi: #Mzizi_Mkavu
SASA SIKIA ILI USIPITWE NA MWENDELEZO WA HADITHI HII #LIKE_PAGE HII USIPITWE NA KIPANDE HATA KIMOJAAA SHARE NIPOST KIPANDE KINACHOFUATA NASUBIRIA #SHARE ZIFIKE 250 NIPOST MWENDELEZO
ILIPOISHIA:
Hakika Shehna alikuwa mrembo wa warembo.
“Haki ya nani Shehna sijakuita,” Mustafa alijitetea kwa kuamini toka aachane naye hakumpigia simu wala kuonana naye.
“Huna kitu unachotaka kuniuliza?” Shehna alimuuliza huku amemkazia macho yaliyozidisha uzuri wake.
SASA ENDELEA...“
Ninacho lakini nilijua tutaonana jioni.”
“Sawa angeniuliza jioni lakini toka ufike una muda gani?”
“Zaidi ya saa nzima.”
“Umeishafanya kazi gani?”
“Bado sijaanza.”
“Kwa nini?”
“Sina kazi nyingi ningefanya wakati wowote.”
“Kwa hiyo Mustafa unataka kunidanganya hata mimi?”
“Kwa nini unasema hivyo?”
“Mustafa toka uingie kuna vitu vinakutatiza na kujikuta muda mwingi ukijiuliza maswali mengi ambayo unaamini mwenye majibu yake ni mimi, uongo?”
“Kweli.”
“Haya niulize.”
“Kwa nini tusizungumze jioni kwa vile huu ni muda wa kazi!”
“Mustafa mi si mjinga kuacha kazi zangu na kuja kukusikiliza, najua leo huwezi kufanya kazi mpaka upatiwe majibu ya maswali yako.”
“Umejuaje nataka kukuuliza?”
“Mustafa muhimu kwa muda huu kujua nimejuaje au kukujibu maswali yako.”
“Samahani Shehna.”
“Mustafa kama nisingekuwa mimi usingemruhusu mtu kuingia ndani, uongo kweli?”
“Kwa baadaye lazima ningewaruhusu.”
“Kwa hiyo niondoke?”
“Ha...hapana.”
“Unajua kuna kitu kimenifurahisha sana leo ambacho nimepanga kukuzawadia, lakini unataka kuniudhi.”
“Shehna samahani kama nitakukosea lakini naamini wewe ni mtu muhimu sana kwangu.”
“Ndiyo maana nipo hapa.”
“Kuna mengi ya kukuuliza nashindwa nianze na lipi.”
“La mkeo.”
“Umejuaje?”
“Mustafa acha kuwa mgeni wa dunia kushtuka kila kitu, uliza ili ujibiwe si kujua nimejuaje.”
Mustafa alizidi kumshangaa Shehna kuyajua yaliyojificha moyoni mwake, alijiuliza yeye ni kiumbe wa aina gani mwenye uwezo wa ajabu kama ule? Hakuwa na jinsi alimueleza aliyoelezwa na mkewe juu ya kumuomba msamaha kwa yote yaliyotokea.
“Mustafa nimemsamehe kwa vile nakupenda lakini mkeo ana kiburi, masharti mengi amekuwa akiyavunja matokeo yake mnatumia fedha nyingi na nguvu nyingi bila mafanikio.”
“Sasa utanisaidiaje?”
“Unataka msaada wangu upi?”
“Bado tunataka mtoto.”
“Mmechelewa.”
“Kivipi?’
“Unakumbuka nilikuambia nini?”
“Vitu vingi, kimoja wapo?”
“Kuhusu kupata mtoto.”
“Si ulisema utanipa mimi kwanza ndipo nikupe wewe.”
“Ni kweli, lakini makosa ya mk
0 comments:
Post a Comment