Imeelezwa kuwa, Ronaldo ameinyakua tuzo hiyo kutokana na mchango wake mkubwa kwa timu ya taifa ya Ureno na kuipeleka kwenye fainali za Kombe la Dunia nchini Brazil na mchango wake mkubwa kwa klabu yake ya Real Madrid katika kuunyakua ubingwa wa Champions League na mataji mengine mwaka jana.
Kwa upande wa wanawake, mchezaji bora wa mwaka alitangazwa Nadile Kessler, na tuzo ya goli bora la mwaka imechukuliwa na James Rodriguez wa timu ya taifa ya Colombia. Kocha wa mwaka ametangazwa, Joachim Low wa Ujerumani, na kwa upande wa kocha bora wa soka la akina dada ni Ralf Kellermann.
0 comments:
Post a Comment